Mambo hayo ambayo ni hatua za kumsaidia mtu
aliyenusurika katika shambulio husika ili kunusuru maisha yake,
yametajwa wakati zikiwapo taarifa za tisho la shambulizi katika miji ya
Dar es Salaam na Mwanza.
Jarida hilo lilifanya mahojiano na wataalamu wa
sayansi ambao walitoa mapendekezo ambayo mtu anaweza kufuata wakati au
baada ya mlipuko na kuwa asilimia 50 ya watu wanaokutwa katika
mashambulizi ya kigaidi hujeruhiwa na wengine kupoteza maisha kwa
sababu hawafahamu jinsi ya kujihami.
Tanzania iliwahi kukumbwa na shambulio la ugaidi
mwaka 1998 wakati Ubalozi za Marekani, jijini Dar es Salaam
ulipolipuliwa na kusababisha vifo vya watu kumi na moja. Shambulio hilo
lilitokea sambamba na lile la ubalozi wa nchi hiyo, Nairobi, Kenya
lililosababisha vifo ya watu 213.
Uvumi zaidi umeendelea kuenea baada ya shambulio
la kigaidi lililotokea wiki iliyopita katika Chuo Kikuu cha Garissa,
Kenya na kuua wanafunzi 148.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mathias Chikawe alisema pamoja na kusikia taarifa hizo, mpaka sasa
Serikali haijaweza kuthibitisha ripoti hizo zinazoenea, lakini inachukua
tahadhari juu ya suala hilo.Kwa Habari Zaidi
No comments:
Post a Comment