
Hayo yalibainishwa na Rais Jakaya Kikwete, wakati akifungua mkutano
wa siku tatu wa dunia kuhusu masuala ya lishe duniani, jana jijini Dar
es Salaam.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, serikali imekuwa na mikakati mbalimbali
ya kukabiliana na utapiamlo nchini ukiwamo wa 2011/12 hadi 2015/2016
ambao umesaidia kupunguza idadi ya watoto wenye utapiamlo kutoka
asilimia 42 mwaka 2010 hadi asilimia 34.7 mwaka uliopita.
Mikakati hiyo pamoja na mambo mengine, inalenga kuweka viini lishe
kwenye vyakula na kwamba tangu kuzinduliwa kwake, takribani watu milioni
20 wamefikiwa na mazao ambayo tayari yamewekewa viini lishe.
Hata hivyo, alisema bado nchi ipo katika safari ndefu katika
kufikia malengo ya milenia ya mkutano wa afya wa dunia na yale ya
Tanzania ya mwaka 2025.
Rais Kikwete alisema wasiwasi wa kutofikiwa kwa malengo hayo ya
kidunia na yale ya kitaifa, unatokana na taifa kuwa na idadi kubwa ya
watoto wenye tatizo la utapiamlo ambao kwa sasa ni takriban milioni 2.7.
Alisema, asilimia 58 ya watoto hao, wanatoka katika mikoa 10 nchini ambayo inakabiliwa na tatizo kubwa la lishe.
Rais Kikwete alisema ushirikiano wa kutosha kati ya serikali na
wadau wengine zikiwamo sekta binafsi katika kukabiliana na suala hilo,
vinginevyo, watoto takriban 580, 687 nchini wapo hatarini kupoteza
maisha ifikapo mwaka 2025.
“Bado kuna njia ndefu kwa Tanzania ili iweze kufikia malengo ya
milenia ya mkutano wa afya wa dunia ya mwaka 2020 na ya Tanzania ya
mwaka 2025 ya kuboresha hali ya lishe,” alisema Rais Kikwete na
kuongeza:
No comments:
Post a Comment