Tuesday, 17 March 2015

Waganga feki wanavyochota mamilioni

BAADHI ya waganga wa kienyeji nchini sasa wamegeuza matatizo ya Watanzania kuwa mitaji yao ya kujipatia mamilioni ya fedha kwa madai kwamba wanawapatia tiba.

Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumamosi umebaini kuwa wengi wa waganga hao wanaojipatia fedha kwa njia ya kuwadaganya wananchi ni wale ambao hawajasajiliwa na Serikali. Moja ya uthibitisho wa kwamba huduma hiyo haramu huwapatia fedha nyingi waganga hao ni kuenea kwa mabango mengi yanayotangaza kuwepo kwa waganga hao.

Katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es Salaam na miji migine mikubwa nchini huwezi kutembea mwendo mrefu bila kukutana na kibao kinamtangaza mganga wa kienyeji kutoka ndani na nje ya nchi.

Miongoni mwa waganga hao, wapo wanaojitangaza kutibu watu walio na matatizo ya nguvu za kiume, wanaotaka kupata utajiri wa haraka, kutibu mwanafunzi ambaye hana akili darasani, kuolewa au kuoa haraka, kumvuta mpenzi aliye mbali, kunenepesha makalio na kurefusha maumbile ya sehemu za siri kwa wanaume na mengineyo.Bofya hapa kwa habari zaidi

No comments:

Post a Comment