Wednesday, 11 March 2015

Vifo visivyo vya lazima katika uzazi vidhibitiwe.

Sensa ya watu nchini Tanzania yaonyesha kuna watu zaidi ya milioni 45 kwa sasa.Idadi hiyo yahitaji mikakati maalum ya kuhakikisha kuwa wanapiga hatua za maendeleo za uhakika.Maendeleo hayo yatafikiwa kama tu watu hao watakuwa na afya njema.

Idadi ya watu imeongezeka mara mbili toka watu milioni 25 mwaka 1990 hadi watu milioni 45 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012. Hali hii, inaleta changamoto kubwa katika utoaji wa huduma bora za afya , huduma za kijamii kama vile maji na elimu hasa kwa kuzingatia kuwa, asilimia 70 ya watanzania vijijini na karibu asilimia 30 ya wanawake walio kwenye umri wa kuzaa hawana elimu.
 
Mbio hizo za kiuchumi , zinaweza kufanikiwa tu iwapo kutakuwa na uwiano wa huduma muhimu na za msingi ikiwemo zile za afya hasa ya uzazi, kwa akina mama,watoto wachanga na watoto chini ya umri wa miaka mitano kufikia mwaka 2035.
 
Mafanikio hayo, yanatakiwa kwenda sambamba na kasi ya kupunguza kama si kuondoa kabisa vifo vya watanzania hasa akina mama,watoto wachanga, watoto chini ya miaka mitano  na watoto waliozaliwa wafu kwa zaidi ya asilimia 80. Hii ina maana ya kuokoa maisha ya watu 60,000 kwa mwaka.
 
Tafiti na takwimu mbalimbali zinaonyesha kuwa, takriban  wanawake 7,900 wa Tanzania hufa kutokana na matatizo ya ujauzito na kujifungua. Watoto 40,000 hufariki katika kipindi cha siku 28 za mwanzo wa maisha yao huku wengine takriban watoto 100,000 hupoteza maisha kabla ya kufika umri wa miaka mitano.Kwa Maelezo zaidi
 

No comments:

Post a Comment