Taarifa zilizoripotiwa jana na gazeti hili zikimkariri mganga mkuu
wa hospitali hiyo zilionyesha kuwa hali ni mbaya na kwamba jitihada za
haraka zinahitajika sasa ili kupunguza changamoto zitokanazo na
mrundikano wa wagonjwa hospitalini hapo.
Inaelezwa kuwa hivi sasa, idadi ya shuka zilizopo katika hospitali
hiyo ni 1,200 wakati mahitaji halisi yatokanayo na idadi kubwa ya
wagonjwa wanaofikishwa na kulazwa hapo kila uchao ni zaidi ya shuka
2,400.
Hili ni tatizo kubwa. Ukweli huu unatokana na ukweli kwamba uwiano
wa shuka zilizopo na wastani wa zile zinazohitajika hauko sawa. Ni kwa
sababu uhaba uliopo unafikia takriban nusu ya shuka zinazohitajika na
hali hiyo siyo nzuri hata kidogo. Bofya hapa kwa habari zaidi
No comments:
Post a Comment