Friday, 27 March 2015

mwanzo Mkakati kuingiza teknolojia tiba ya mfumo wa fahamu Tanzania

Umakini kwa mara nyingine tena umewekwa katika uhitaji wa wataalamu zaidi na kuboresha miundombinu ndani ya sekta ya utabibu wa upasuaji wa mfumo wa fahamu.
Hii inakuja baada ya ziara ya hivi karibuni na timu ya madaktari kutoka Hospitali ya Apollo nchini India. Madaktari ambao walikuwa nchini kwa lengo la kujenga uhusiano unaoendelea kati ya hospitali hiyo na Tanzania.
Walipata fursa ya kutembelea taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na maboresho ya ujuzi kwa wauguzi ambao walipata mafunzo kutoka Hospitali ya Apollo.
Matibabu ya magonjwa ya mfumo wa fahamu ni mada nyeti yenye matatizo mbalimbali kama yakifanyika kwa namna isiyo sahihi.
Kuvurugika kwa mishipa ya fahamu ni ugonjwa ambao unatokea katikati na pembeni ya mfumo wa neva. Ambapo kimuundo, upungufu wa kemikali au umeme kutokuwa sawa katika ubongo, uti wa mgongo au mishipa mingine, inaweza kusababisha dalili za aina mbalimbali.
Tanzania kwa sasa kuna madaktari saba wa mfumo wa fahamu ambao wote kwa sasa ni watendaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kutokana na kutokuwapo kwa kumbukumbu sahihi za matatizo ya mifumo ya neva, hakuna uhakika wa kiwango ambacho tatizo hili linawakumba Watanzania. Hii ni tofauti na wenzao nchini India.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Sayansi ya Mfumo wa Fahamu wa Hospitali ya Apollo iliyopo Bangalore, India, Profesa Krishna Kambadoor anasema takwimu za wanaougua India inaweza ikawa sawa na Tanzania.
Profesa Krishna anasema mlo usio kamili husababisha matukio ya magonjwa ya kisukari na matatizo yanayoambatana katika sehemu za mwili ikiwa ni pamoja na kupoteza uwezo wa hisia.
Matatizo haya anasema ni pamoja na kuongezeka idadi ya magonjwa yanayohusiana na umri mkubwa miongoni mwao, yakiwamo mishipa ya fahamu na moyo kwa ujumla.
Anasema hospitali za Apollo zinatarajia kuleta jopo la madaktari wataalamu wa mfumo wa fahamu ili kuisaidia Tanzania kubaini ukubwa wa tatizo na jinsi ya kukabiliana nalo. “Hii ni hatua ambayo itatazama utengenezaji wa vituo mtaalamu ambapo itaboresha huduma na kuongeza wataalamu wa afya hapa nchini,” anasema.
Profesa Krishna anasema hospitali za Apollo zinatazamia kuleta mapinduzi ya tiba kwa magonjwa ya mfumo wa fahamu. Anasema anahisi hilo linawezekana kwa sababu miaka 20 iliyopita, India ilikuwa na mazingira kama yanayoonekana kwa sasa nchini ya kutokuwa na takwimu sahihi.
“India kama Tanzania ilikuwa katika hali kama hii miongo mitatu iliyopita na tangu wakati imeingia kutoka Taifa linaloendelea na kuwa karibu sawa na mataifa yaliyoendelea,” anasisitiza akifafanua:CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment