Thursday, 19 March 2015

Muuguzi anayedaiwa kutekwa wiki iliyopita apatikana, ahojiwa na polisi

Muuguzi wa Hospitali ya Mwananyamala, Pili Amiri aliyetekwa Machi 12, amepatikana usiku wa kuamkia jana baada ya watekaji hao kudaiwa kumtupa katika pori moja lililoko Dar es Salaam.

Hata hivyo, gazeti hili lilishindwa kufanya mahojiano na muuguzi huyo jana kwa kuwa alikuwa akihojiwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, kuanzia saa nne asubuhi hadi mwandishi alipoondoka kituoni hapo saa 11 jioni.
Kwa mujibu wa shangazi yake Pili, Fatuma Mbasa, muuguzi huyo alirudi nyumbani saa 10 alfajiri jana akiwa katika hali ya kulewa na makovu kadhaa shingoni.
 
“Inaonekana walimpa dawa za kulevya kwa sababu alikuwa kama teja, hajiwezi na ana majeraha kadhaa na alikuwa akilalamika kuwa na maumivu shingoni,” alisema Mbasa.Soma Zaidi

No comments:

Post a Comment