Thursday, 11 June 2015

Mimba za utotoni, nani wa kumfunga paka kengele?

Kila kukicha kumekuwa na kesi za migogoro ya ardhi, mirathi na hata kesi za wazazi kuozesha mabinti zao wakiwa na umri mdogo licha ya suala hilo kupigiwa kelele muda mrefu.
Hiyo ni changamoto inayolikabili taifa, huku baadhi ya watu wakiliona kuwa ni jambo la kawaida na hulipuuza wakati wengine wanalikemea.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Haki za Binadamu Duniani(Amnesty) iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Tanzania ni moja ya nchi zinaoongoza kwa matukio ya mimba za utotoni.
Takwimu zinaonyesha kuwa, kwa siku, watoto 16 wanapachikwa mimba za utotoni.
Kwa mujibu wa wataalamu, hali hiyo imekuwa ikiendelea kwa muda mrefu na kwa asilimia kubwa inazorotesha maendeleo ya mtoto wa kike.
Ili kumwokoa mtoto wa kike kutoka janga hilo, jitihada mbalimbali zimefanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha inawaokoa hasa wale ambao tayari wameshatumbukia katika dimbwi hilo.
Utafiti uliofanywa hivi karibuni na Chama chaWaandishi wa Habari Wanawake (Tamwa), unaonyesha kuwa katika kipindi cha mwaka 2012/2013, matukio 228 ya mimba na matukio 42 ya ndoa za utotoni yaliripotiwa.
Hata hivyo, mimba na ndoa za utotoni zimetajwa kuwa miongoni mwa vikwazo vinavyowapata watoto wa kike wa Tanzania, tatizo ambalo bado ni kubwa katika baadhi ya maeneo ya Tanzania Bara na Visiwani.
Mimba za utotoni na ukatili
Kwa kiasi kikubwa tatizo hilo linakwenda sanjari na ukatili wa kijinsia ambapo kwa Tanzania Visiwani hali hiyo imeonekana zaidi katika Mkoa wa Kusini Pemba na Wilaya ya Kati Unguja, huku upande wa Tanzania Bara maeneo yenye ukatili dhidi ya wanawake pamoja na mimba za utotoni yakitajwa kuwa ni Wilaya za Kahama, Tarime, Sengerema, Newala, Mbulu, Bunda, Nkasi, Babati, Chunya, Dodoma, Bariadi, Busega na Singida vijijini.
Bokhe Odhiambo (31), mkazi wa Tarime mkoani Mara, anasema kuwa vitendo vya ukatilli dhidi ya wanawake ndani ya ndoa na mimba za utotoni kwa watoto wa kike ni mambo ya kawaida na jamii inaonekana kuwa haina muda wa kuyakemea.
“Kupigwa au kufanyiwa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake ndani ya ndoa, migogoro ya ardhi na mimba za utotoni kwa watoto wa kike ni mambo ya kawaida tu kwenye jamii yetu licha ya wasaidizi wa kisheria kutoa elimu,” anssema Odhiambo.Kwa habari zaidi

No comments:

Post a Comment